728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, June 13, 2017

    Lyon yaitajia Arsenal bei ya Lacazette


    Lyon,Ufaransa.

    LYON imeiambia Arsenal kuwa italazimika kukata pochi nene kama kweli inataka kumsajili mshambuliaji wake mahiri,raia wa Ufaransa Alexandre Lacazette.

    Kwa mujibu wa gazeti la Telegraph,Lyon inataka ilipwe kitita cha €55m (£48.7m) kama ada ya awali kisha €12m (£10.6m) kama ada ya nyongeza kwa ajili ya mshambuliaji huyo mwenye miaka 26.

    Dai hilo limetolewa jana Jumatatu na Rais wa Lyon,Jean-Michael Aulas ambaye mapema wiki iliyopita alifanya kikao na ujumbe wa Arsenal uliofika kumuona ukiongozwa na kocha Arsene Wenger pamoja na Mtendaji Mkuu wa klabu,Ivan Gazidis.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Lyon yaitajia Arsenal bei ya Lacazette Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top