728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 05, 2016

    AFCON IMEKAMILIKA TIMU 16 ZAFUZU,KIPUTE KUANZA JANUARI 16,SENEGAL YAWEKA REKODI

    Cairo,Misri.

    HATIMAYE timu 16 zitakazoshiriki michuano ya kuwania ubingwa wa mataifa huru ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Gabon zimefahamika baada ya michezo ya mwisho kuchezwa jana Jumapili.

    Ukiachana na wenyeji Gabon ambao wamefuzu moja kwa moja bila kumwaga jasho.Timu nyingine ambazo zimefuzu na kukamilisha idadi ya timu 16 ni:

    Algeria,Burkina Faso , Cameroon,Cote d’Ivoire

    DR Congo, Egypt, Ghana , Guinea Bissau , Mali ,Morocco, 

    Senegal , Togo , Tunisia, Uganda na Zimbabwe.

    Uganda na Togo zimefuzu zikiwa kama washindwa bora (Best Losers) baada ya kumaliza katika nafasi za pili katika makundi A na D.

    Uganda imemaliza ikiwa na alama 13,Togo imemaliza ikiwa na alama 11.Senegal imefuzu katika michuano hiyo ikiweka rekodi ya kuwa timu pekee iliyoshinda michezo yake yote sita ya hatua ya makundi.Guinea-Bissau imefuzu kwa mara ya kwanza.

    Michuano ya AFCON itaanza kutimua vumbi lake Januari 14 nchini Gabon.

    MATOKEO YOTE YA MICHEZO YA JUMAPILI

    Malawi 1-0 Swaziland
    Uganda 1-0 Comoros
    Burkina Faso 2-1 Botswana
    Zambia 1-1 Kenya
    Congo 1-0 Guinea Bissau
    Equatorial Guinea 4-0 South Sudan
    Guinea 1-0 Zimbabwe
    DR Congo 4-1 Central Africa
    Mali 5-2 Benin
    Niger 0-0 Burundi
    Togo 5-0 Djibouti
    Tunisia 4-1 Liberia
    Morocco 2-0 Sao Tome
    Algeria 6-0 Lesotho

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: AFCON IMEKAMILIKA TIMU 16 ZAFUZU,KIPUTE KUANZA JANUARI 16,SENEGAL YAWEKA REKODI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top