728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, September 10, 2016

    VPL:YANGA,AZAM FC ZAVUNA POINTI 3 DAR NA MBEYA


    Dar Es Salaam,Tanzania.

    MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara,Yanga SC,wameitoa nishai Majimaji FC ya Songea baada ya jioni ya leo kuichapa mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Uhuru,Dar Es Salaam.

    Mabao ya Yanga SC yamefungwa na Deus Kaseke dakika ya 19 na Amissi Tambwe aliyefunga mabao mawili dakika za 79 na 85.

    Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo uliochezwa huko Sokoine,Mbeya,Azam FC imechomoza na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: VPL:YANGA,AZAM FC ZAVUNA POINTI 3 DAR NA MBEYA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top