728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, June 08, 2015

    VERMAELEN AIKOSESHA ARSENAL MKWANJA WA MAANA

    Barcelona,Hispania.

    Klabu ya Arsenal imekosa kitita cha £3m licha ya klabu ya Barcelona kutwaa ubingwa wa Ulaya mapema juzi jumamosi.

    Arsenal ilitarajia kupokea bonasi ya £3m kufuatia mauzo ya mlinzi wake Thomas Vermaelen kwenda klabu ya Barcelona mwezi agosti mwaka jana.

    Katika usajili huo ulioigharimu Barcelona ada ya £15m kulikuwa na kipengere ambacho kiliipa nafasi klabu ya Arsenal kupata bonasi hiyo iwapo  Barcelona itatwaa ubingwa wa Ulaya ikiwa na Vermaelen kama mmoja wa wachezaji waliotia mguu uwanjani yaani kucheza japo mchezo mmoja pekee.

    Mpaka Barcelona inatwaa ubingwa huo Vermaelen ameshindwa kucheza mchezo wowote licha ya mara kadhaa kuwa miongoni mwa wachezaji wa akiba.Kufuatia hali hiyo klabu ya Arsenal imekosa mkwanja huo wa uhakika.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: VERMAELEN AIKOSESHA ARSENAL MKWANJA WA MAANA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top