728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, June 17, 2015

    POMBE SIYO CHAI:VIDAL ACHUNGULIA KIFO USIKU WA KUAMKIA LEO.

    Habari na Paul Manjale
                                        
    Kiungo wa klabu ya Juventus na timu ya taifa ya Chile Arturo Vidal 28 amenusurika kifo jana jumanne usiku baada ya gari yake kugongana na gari jingine
    katika jiji la Santiago.

    Vidal akiwa na mkewe Maria Teresa Matus wakitoka kula starehe katika Casino moja maarufu walikutwa na ajari hiyo baada ya Vidal kushindwa kulidhibiti gari alilokuwa akiliendesha kutokana na kuzidiwa na pombe.

    Afisa mmoja wa polisi aliyejulikana kwa jina la Ricardo Gonzalez alisema "Dereva wa gari jekundu alikuwa amelewa sana"

    Vidal alikimbizwa katika hospital ya San Luis de Buin kupata matibabu baada ya kupata majeraha madogo madogo.

    Baadae nyota huyo wa Juventus alionekana akiwa ndani ya gari la porisi akipelekwa kituoni kwa mahojiano zaidi.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: POMBE SIYO CHAI:VIDAL ACHUNGULIA KIFO USIKU WA KUAMKIA LEO. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top