728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, June 12, 2015

    KOPUNOVIC KUREJEA KUIFUNDISHA SIMBA

                                      

    SIMBA imefanya uamuzi mgumu kwa kumrudia kocha wake, Mserbia
    Goran Kopunovic na huenda akatua nchini muda wowote kuanzia sasa kuendelea na kibarua chake.

    Kocha huyo aliithibitishia Mwanaspoti jana Jumatano kwamba amezungumza na Simba juzi na jana jioni walikuwa kwenye makubaliano ya mwisho ambayo yalikuwa na asilimia kubwa ya kukamilika.
    Habari za ndani zinasema kwamba Simba imempa Kopunovic ofa ya mshahara kiasi cha dola 6,500 sawa na Sh14 milioni kwa mwezi na pesa ya usajili dola 15,000 ambazo ni sawa na Sh32 milioni ili arudi kuifundisha klabu hiyo.

    Kopunovic ameikubali ofa ya mshahara, lakini utata ukawa kwenye pesa ya usajili baada ya kutaka apewe dola 25,000 ambazo ni sawa na Sh53 milioni kwa makubaliano ya mkataba wa mwaka mmoja.
    Chanzo ndani ya Simba kilisema baada ya kutofautiana, Simba walimwahidi Kopunovic atapewa jibu jana Jumatano baada ya uongozi wa klabu kukubaliana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KOPUNOVIC KUREJEA KUIFUNDISHA SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top