728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, June 08, 2015

    KOMBE LA DUNIA LA WANAWAKE:UJERUMANI YAGONGA MTU 10-0

    Habari na Paul Manjale

    Kombe la dunia la wanawake lilianza kutimua vumbi lake jana nchini Canada.

    Katika mchezo wa ufunguzi wenyeji Canada waliifunga China goli 1-0 kupitia mkwaju wa penati uliopigwa kiufundi na nahodha wake Christine Sinclair baada ya mlinzi wa China Zhao Rong  kumfanyia madhani Adriana Leon wa Canada.

    Kutoka kundi B:Timu ya taifa ya Ujerumani imetoa onyo baada ya kuwatandika wawakilishi wa Afrika timu ya Ivory Coast kwa jumla ya magoli 10-0 katika mchezo ukiopigwa katika dimba la Lansdowne,Ottawa.

    Magoli ya Ujerumani yalifungwa na Celia Sasic 3', 14', 31'; Anja Mittag 29', 35', 64'; Simone Laudehr 71'; Sara
    Daebritz 75'; Melanie Behringer 79';Alexandra Popp 85'

    Katika mchezo mwingine wa kundi hilo Norway iliibuka na ushindi wa goli 4-0 dhidi ya Thailand.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KOMBE LA DUNIA LA WANAWAKE:UJERUMANI YAGONGA MTU 10-0 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top