728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, July 10, 2015

    KISA MESSI!!HANS POPPE ASUSA KULA KEKI,KUNYA MAJI YA AZAM

    Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe ametoa kali baada ya kusema amesusia kununua vitu vinavyotengenezwa na kampuni ya Azam FC.
    Hans Poppe amesema hatakuwa akinywa maji ya Azam wala kula kesi za Azam kwa madai wamewafanyia ‘uhuni”.

    Hans Poppe ameyasema hayo leo wakati akihojiwa la E FM Radio kwa madai Azam FC wamefanya hila kuhakikisha wanampata kiungo Ramadhani Singano ‘Messi’ kwa hila.

    “Wamemsajili Messi kwa ujanja, wameshinikiza hili suala ili wampate kijanja. Nasema mimi sasa sitakula keki zao wala kunywa maji yao.

    “Ndiyo, nafanya hivyo ili kupunguza nguvu. Maana kama tunanunua vitu vyao tunawapa nguvu halafu wanatudhulumu,” alisema.

    Messi ametua Azam FC baada ya kamati ya maadili na hadhi za wachezaji ya TFF kuvunja mkataba wake.

    Simba wamekuwa wakilaumu uvunjwaji huo wa mkataba unaonyesha kuwa wa mipango.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KISA MESSI!!HANS POPPE ASUSA KULA KEKI,KUNYA MAJI YA AZAM Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top