728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, July 19, 2015

    XAVI ASEMA YEYE NDIYE ALIYEITOSA BARCA


    Kiungo nguli Xavi Hernandez amefichua kwamba Barcelona ilitaka abakie Nou Camp mpaka 2018 lakini yeye akachomoa na kuamua kujiunga na Al-Sadd ya Qatari mara baada ya mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa dhidi ya Juventus.

    Akiongea na kituo cha redio cha RAC1, Xavi 35 amesema: “Josep Maria Bartomeu alikuja nyumbani kwangu kunitaka nibaki Barca.Kabla ya hapo alishanishawishi pamoja na [Mkurugenzi wa zamani wa michezo Andoni] Zubizarreta na [kocha] Luis Enrique,wakitaka nibaki kwa mwaka mmoja zaidi.

    “Kipindi hiki walikuja tena wakitaka nibakie mpaka 2018.Sikuwakubalia kwa kuwa niliona wakati wangu kuondoka umefika.Hivyo nikaondoka".


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: XAVI ASEMA YEYE NDIYE ALIYEITOSA BARCA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top