728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, July 31, 2015

    BASATA IMEMFUNGIA SHILOLE MWAKA MMOJA, HAKUNA KUFANYA MUZIKI

    Baraza la sanaa Tanzania (BASATA) limemfungia Shilole kutojihusisha na kazi yoyote ya sanaa kwa muda wa mwaka mmoja.
     
    Barua iliyoifikia soka extra ambayo imeandikwa kutoka BASATA imesema  Tarehe 9 May 2015 ukiwa katika onyesho lako la muziki Ubelgiji ulicheza uchi mbele ya hadhira ya wapenda sanaa za Tanzania hivyo kudhalilisha utu wako na jamii ya kitanzania kimaadili
    Shilole 2BASATA ilipata habari zako, kumbuka pia October 2013 BASATA
    lilikuonya na ukakiri kwa kuomba msamaha tabia yako ya kucheza bila kuzingatia maadili uwapo jukwaani, BASATA ilikupa nafasi ya kutoa maelezo kwanini usichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kitendo chako lakini umekaidi kutoa maelezo yako‘ – BASATA
    ShiloleBaraza limejiridhisha kwamba ulikiuka maadili ya kazi ya sanaa kwenye onyesho lako huko Ubelgiji makusudi na umekiuka sheria kwenye ibara ya 30 (2) ya katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kwa kuvunja maadili ya jamii ya Mtanzania hivyo baraza linakusimamisha kujishughulisha na kazi za sanaa nchini na nje ya nchi kwa mwaka mmoja, kufanya kinyume na hayo kutapelekea kupewa adhabu zaidi pamoja na yeyote utakaeshirikiana nae ‘ – BASATA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BASATA IMEMFUNGIA SHILOLE MWAKA MMOJA, HAKUNA KUFANYA MUZIKI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top