728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, July 31, 2015

    MAVUGO NDIYO BASI TENA SIMBA

     
    HUENDA Simba ikawa inacheza mchezo wa pata potea kwa straika, Laudit Mavugo wa Vital’O baada ya klabu hiyo ya Burundi kuweka bayana kwamb
    a kama Simba haitaweka mzigo mezani basi isitarajie kumpata.
    Simba ilikurupuka na kwenda kufanya mazungumzo na Mfungaji Bora huyo wa Ligi Kuu Burundi, kisha kusaini naye mkataba wa miaka miwili na kumpa chake dola 10,000 (Sh20 milioni) kati ya dola 20,000 walizokubaliana.
    Hata hivyo Rais wa Vital’O, Bikolimana Benjamin, alisema klabu hiyo haipo tayari kumwachia Mavugo kama Simba haitatoa dola 100,000 (Sh200 milioni) ili kuvunja mkataba wa mwaka mmoja uliobaki baina yao na straika huyo.
    Msimamo huo wa umeiweka Simba katika wakati mgumu ambapo sasa taarifa za ujio wa mchezaji huyo ni za kupigwa kalenda kila siku huku ikielezwa kwamba tayari tiketi ya kuja nchini ilitumwa kwa straika huyo ambaye ameonyesha mapenzi dhahiri ya kutua Msimbazi.
    Simba ilifanya mazungumzo na Mavugo na kukubaliana katika kila kitu ambapo ingempatia dola 20,000 (Sh 40 milioni) kama ada ya usajili na tayari walishatoa dola 10,000 (Sh 20 milioni) kama kishika uchumba.
    Benjamini aliliambia Mwanaspoti akisema: “Tulifanya mazungumzo ya awali na Simba, lakini mpaka sasa bado hawajatupa jibu kuhusiana na fedha hiyo, walituambia kwamba wangekuja jana (juzi) au leo (jana) ila mpaka sasa hatujamwona kiongozi wao yeyote.
    “Tuliwaambia watulipe dola 100,000, wakilipa hizo tutamwachia Mavugo ama timu yoyote ambayo itakuwa tayari kwa hilo maana makubaliano waliyofanya na Mavugo sisi hatuyatambui.
    “Linalotushangaza wamemalizana na mchezaji wakati bado ana mkataba na sisi.”
    Taarifa za awali zilieleza kwamba Vital’O ilitaka ipewe dola 60,000 (Sh 120 milioni) kama ada ya usajili ya straika huyo lakini Simba ilikuwa tayari kutoa dola 30,000(Sh 60 milioni) ambazo sasa wamezigomea na kupandisha hadi dola hizo 100,000.
    Rais wa Simba, Evans Aveva ambaye alikiri juu ya shinikizo hilo, lakini alidai fedha hizo za dola 100,000 ni nyingi mno kwao.

    “Fedha hiyo ni nyingi mno na hatuna uwezo wa kuitoa ila tunataka kuonana na kiongozi wa Shirikisho la Soka la Burundi ambaye amekuja hapa ili tuone yeye atatusaidiaje juu ya hilo, barua yao ya mwanzo hawakutaja kiasi hicho tunashangaa wamebadilika ghafla,”.
    Kwa upande wa Mavugo ambaye anaonekana kuwa na kiu ya kukipiga Msimbazi alisema: “Mimi nipo tayari kwa safari muda wowote nitakapoambiwa mambo yao yamekamilika kati ya viongozi wa Simba na Vital’O.
    (mwanaspoti)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAVUGO NDIYO BASI TENA SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top