728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, July 20, 2015

    RATIBA YA MECHI ZA KAGAME LEO NA KESHO HII HAPA!!

    Michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea kutimua vumbi katika viwanja viwili vya Taifa na Karume vilivyopo jijini Dar es salaam, inaendelea leo kwa michezo miwili itayopigwa Uwanja wa Taifa.

    Vinara wa kundi A timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya, leo jumatatu watashuka dimbani kucheza na timu ya KMKM kutoka Visiwani Zanzibar. 

    Gor Mahia ambayo ilipata ushindi wa mabao 2- 1 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Yanga, itakutana na KMKM ambayo iliibuka na ushindi wa bao 1 – 0 dhidi ya timu ya Telecom ya Djibout, mchezo utakaochezwa saa 10 jioni Uwanja wa Taifa.

    Mchezo wa kwanza utazikutanisha timu za Telecom ya Djibout dhidi ya Khartoum-3 kutoka nchini Sudan, ambayo itakua ikicheza mchezo wake wa kwanza.

    Kesho Jumanne kutakuwa na michezo mitatu ambapo Al Shandy watacheza na LLB katika kundi B saa 8 mchana uwanja wa Taifa, Heegan FC dhidi ya APR uwanja wa Karume saa 10 jioni, Malakia dhidi ya Azam kundi C Uwanja wa Taifa saa 10 jioni.
    Jumatano mabingwa mara tano wa michuano ya Cecafa Kagame Cup, timu ya Yanga SC watacheza dhidi ya Telecom ya Djibout saa 10 jioni uwanja wa Taifa, KCCA wakicheza na Adama City saa 10 jioni uwanja wa Karume, na Khartoum wakicheza mchezo wa awali saa 8 mchana uwanja wa Taifa dhidi ya KMKM.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RATIBA YA MECHI ZA KAGAME LEO NA KESHO HII HAPA!! Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top