728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, July 27, 2015

    BEKI AZAM FC:BINGWA KAGAME KAMA SIYO YANGA,GOR MAHIA BASI SISI

    Beki tegemeo wa Azam FC, Pascal Serge Wawa, raia wa Ivory Coast, amezitazama timu zote zinazoshiriki michuano ya Kombe la Kagame na kutamka kuwa, kama si timu yake ya Azam FC, basi ubingwa utabebwa na Yanga au Gor Mahia.

    Michuano hiyo imefikia hatua ya robo fainali ambayo itaanza kesho Jumanne.
    Mpaka sasa, Gor Mahia wamecheza michezo miwili na kufunga mabao matano, hivyo wanaonekana wana njaa na ubingwa huo. Yanga wao walianza kwa kipigo katika mchezo wa kwanza, lakini bado wana matumaini ya kufanya vizuri.

    Beki huyo aliyetokea Al Merreikh ya Sudan, amesema kuwa, Yanga na Gor Mahia wanaonekana kuwa na upinzani mkubwa na wanacheza kwa kasi na malengo. Alisisitiza kama wataendelea na moto huo, wana nafasi kubwa ya kuchukua ubingwa.

    “Mashindano bado ni magumu, sisi tumeshinda na tuna nafasi ya kupata mafanikio makubwa ya kupata ubingwa, ingawa ni mapema kusema hivyo.
    “Ukiachana na sisi, naziangalia Yanga na Gor Mahia kama timu tishio. Zina wachezaji wazuri na zinacheza kwa malengo.

     Hakika kama watakuwa na kasi hii waliyoanza nayo, wanaweza kufanikiwa kuchukua ubingwa,”

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BEKI AZAM FC:BINGWA KAGAME KAMA SIYO YANGA,GOR MAHIA BASI SISI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top