728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, July 26, 2015

    ARSENAL YATWAA UCHAMPION WA KOMBE LA EMIRATES KWA MARA YA NNE,WALCOTT AENDELEA KUWA MWIBA,CECH NI MATAJI TU



    Klabu ya Arsenal imefanikiwa kutwaa kombe la Emirates baada ya kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya klabu ya Wolfsburg katika mchezo mkali ulioisha hivi punde.

    Arsenal ikicheza katika dimba lake la nyumbani la Emirates ilipata goli hilo dakika ya 50 kupitia kwa mshambuliaji wake Theo Walcott aliyeunganisha vyema pasi ya mshambuliaji kinda Jeff Reine-Adelaide.

    Ubingwa huu ni wa nne kwa Arsenal tangu michuano hiyo ilipoanza kutimua vumbi lake mwaka 2007 na wa kwanza tangu 2010.

    Katika mchezo wa awali klabu ya Villarreal iliibuka na ushindi baada ya kuwafunga mabingwa wa zamani wa Ufaransa Olympique Lyon kwa goli 2-0.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ARSENAL YATWAA UCHAMPION WA KOMBE LA EMIRATES KWA MARA YA NNE,WALCOTT AENDELEA KUWA MWIBA,CECH NI MATAJI TU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top