728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, July 31, 2015

    USAJILI ULIOKAMILIKA:SUNZU ATUA LILLE,BENNACER ASAINI MIAKA MITANO ARSENAL,MUTU,ZOKORA WAPATA SHAVU FC PUNE



    Sunzu:Mlinzi wa kimataifa wa Zambia Stoppila Sunzu amejiunga na klabu ya Lille ya Ufaransa kwa uhamisho wa mkopo akitokea klabu ya
    Shanghai ya China.

    Mbemba:Klabu ya Newcastle United imemsajili mlinzi wa Anderletch Chancel Mbemba,20 kwa ada ya £8.5m 
     Mutu:Mshambuliaji Mromania Adrian Mutu 36 pamoja na kiungo Didier Zokora 34 wamejiunga na klabu ya Fc Pune ya India kwa ajili ya msimu mpya wa ligi ya nchi hiyo 
     Gomez:Klabu ya Besiktas ya Uturuki imemsajili kwa mkopo mshambuliaji Mario Gomez,30 toka klabu ya Fiorentina.Akifanya mahojiano baada ya uhamisho huo kukamilika Gomez amesema ametua Besiktas ili arejeshe makali yake na hatimaye arejewe katika kikosi cha timu ya taifa ya Ujerumani.
    Chiriches:Klabu ya Napoli ya Italia imemsajili mlinzi Vlad Chiriches,25 toka klabu ya Tottenham kwa ada ya £4.5m.Chiriches ametua Napoli baada ya kushindwa kupata namba katika kikosi cha kwanza cha Tottenham kinachonolewa na Mauricio Pochettino. 

    Bennacer:Klabu ya Arsenal imemsajili kinda Mfaransa Ismael Bennacer 18 toka klabu ya Arles-Avignon kwa ada ya £150,000.Bennacer anacheza nafasi ya kiungo mshambuliaji.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: USAJILI ULIOKAMILIKA:SUNZU ATUA LILLE,BENNACER ASAINI MIAKA MITANO ARSENAL,MUTU,ZOKORA WAPATA SHAVU FC PUNE Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top