728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, July 30, 2015

    SIMBA YAISHIKA PABAYA YANGA




    SIMBA ilitaka kushiriki Kombe la Kagame la mwaka huu, lakini Yanga ikaanzisha chokochoko ikitishia kujitoa kama Mnyama angeingizwa.
    Lengo la Jangwani lilikuwa kuhakikisha
    inafikia rekodi ya wapinzani wao hao ya kutwaa mara nyingi mataji ya michuano hiyo.
    Simba ndiyo mabingwa wa kihistoria wakiwa wamenyakua mataji sita tangu michuano hiyo ilipoanzishwa mwaka 1974 wakati Yanga imefanya hivyo mara tano sawa na Gor Mahia, AFC Leopards na Tusker zote za Kenya.
    Hata hivyo hali haikuwa kama ilivyotarajiwa jana Jumatano kwani mastraika wake nyota; Amissi Tambwe, Donald Ngoma na Geofrey Mwashiuya walishindwa kufurukuta mbele ya Azam na timu hiyo kutolewa katika robo fainali kwa mikwaju ya penalti 5-3.
    Yanga ilikwama katika pambano hilo lililochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam baada ya kumaliza dakika 90 huku ikibanwa kila kona.
    Baada ya mwamuzi, Davies Omweno, kuamuru mikwaju hiyo ndipo Yanga ikajikuta ikipoteza penalti moja iliyopigwa kidhaifu na beki wake, Mwinyi Haji.
    Azam ilipata penalti zake kupitia Kipre Tchetche, John Bocco, Himid Mao, Sergie Wawa na Aggrey Morris, huku Salum Telela, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Geofrey Mwashiuya wakifunga kwa upande wa Yanga ambayo haikupiga penalti ya mwisho.
    Azam iliyoungwa mkono na mashabiki lukuki wa Simba, ilionyesha dhamira ya kusonga mbele kwa kuibana Yanga karibu muda wote wa mchezo.
    Mabeki wa kati wa Azam Aggrey Morris na Sergie Wawa walimdhibiti vilivyo straika mpya wa Yanga, Donald Ngoma kiasi cha kutokuwa na makeke katika muda wote.
    Kwenye penalti Mwinyi alizamisha jahazi la Yanga kwa mkwaju wake kudakwa na kipa Aishi Manula na safari ya Yanga kumalizikia hapo.
    Kwa ushindi huo Azam itakwaana na KCCA kesho Ijumaa katika nusu fainali baada ya Waganda hao kushinda mapema jana mchana dhidi ya Al Shandy kwa mabao 3-0.
    Mabao ya KCCA katika mechi hiyo yalitumbukizwa wavuni na Ochaya Joseph, Matovu Farouq na Tom Masiko. Azam itakutana na KCCA ikiwa ni mara ya pili, kwani zote zilikuwa kundi moja na katika mchezo wao Waganda walikubali kipigo cha bao 1-0.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SIMBA YAISHIKA PABAYA YANGA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top