728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, June 15, 2015

    EURO 2016:ENGLAND YAUA,WILSHERE APIGA MBILI

    Ljubljana,Slovenia.
                                          
    Timu ya taifa ya England imeendelea kuisogelea tiketi ya michuano ijayo ya Euro 2016 baada ya usiku wa leo kuibuka na ushindi wa goli 3-2 dhidi ya timu ya taifa ya Slovenia huko Ljubljana.

    Wenyeji Slovenia walipata magoli
    yao kupitia kwa wachezaji wake  Milivoje Novakovic na Nejc Pecnik huku England ikipata magoli yake kupitia kwa kiungo Jack Wilshere aliyefunga magoli 2 na Wayne Rooney aliyefunga goli 1.

    Baada ya magoli hayo Wishere ambaye wakuwahi kufunga goli lolote katika michezo 27 anaingia katika orodha ndefu ya viungo wa England waliowahi kufunga magoli wakiwa na timu yao ya taifa.

    Bobby Charlton magoli 49 akicheza kama kiungo,David Beckham magoli 14,Frank Lampard magoli 29 katika michezo106,Steven Gerrard magoli 21 katika michezo114.Jack Wilshere magoli 2,Andros Townsend magoli 2 na James Milner 1,David Platt magoli 27 kati ya mwaka 1989 na 1996,Bryan Robson magoli 26 katika kipindi cha miaka nane.

    Kufuatia ushindi huo England imendelea kuongoza kundi E ikiwa na alama 18.

    Matokeo mengine ya michezo mingine ya Euro.......
    FT Ukraine 3-0Luxembourg
    FT Belarus 0-1 Spain
    FT Slovakia 2-1 FYR Macedonia
    FT Estonia 2-0 San Marino
    FT Slovenia 2-3 England
    FT Lithuania 1-2 Switzerland
    FT Liechtenstein 1-1 Moldova
    FT Russia 0-1Austria
    FT Sweden 3-1Montenegro
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: EURO 2016:ENGLAND YAUA,WILSHERE APIGA MBILI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top