728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, July 07, 2015

    CHELSEA YATENGA DONGE NONO KUHAMIA WEMBLEY

                                              Tokeo la picha la WEMBLEY STADIUM
    Chelsea wako tayari kutoa kiticha cha m £11m kwa mwaka ili kuutumia uwanja wa Wembley Stadium kwa misimu mitatu wakati uwanja
    wake wa Stamford Bridge ukifanyiwa upanuzi toka watazamaji 42,000 mpaka 60,000.
                                           Tokeo la picha la WEMBLEY STADIUM
    Gazeti la Times  limeripoti Chelsea,ambao watahitaji uwanja wa muda msimu wa  2017-18 tayari wameifikisha ofa kwenye bodi ya usimamizi ya uwanja wa Wembley.

    Mbali na Chelsea,klabu ya Tottenham nayo iko katika mbio za kutaka kuutumia uwanja huo na tayari imeandaa ofa ya £8m ili kutimiza lengo hilo na kupisha marekebisho yanayotakiwa kufanywa katika uwanja wake wa White hart Lane.
     Tokeo la picha la WEMBLEY STADIUM
    The Times limeendelea kutanabaisha kuwa licha ya ofa hizo kubwa lakini bado bodi ya usimamizi wa Wembley haijaamua iwapo itaupangisha uwanja huo ama la.
    Ikiwa mpango huo utakwama Chelsea itahamia katika uwanja wa Twickenham ambao ni maarufu kwa mchezo wa Rugby.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHELSEA YATENGA DONGE NONO KUHAMIA WEMBLEY Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top