728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, March 30, 2016

    UFARANSA YAICHAPA URUSI 4-2,URENO YAITAMBIA UBELGIJI

    Saint-Denis,Ufaransa.

    Ufaransa imeshinda mchezo wake wa kwanza tangu tangu ilipokumbwa na shambulio la ugaidi Novemba 13 mwaka jana baada ya jumanne usiku kuitandika Urusi kwa mabao 4-2 katika mchezo wa kirafiki uliopigwa huko Stade de France,Saint-Denis. 

    Magoli yaliyoipa Ufaransa ushindi huo mnono yamefungwa na N’Golo Kante (8'),Andre-Pierre Gignac (38),Dimitri Payet (64) na Kinglsey Coman (76) huku yale ya Urusi yakifungwa na Alexander Kokorin (56 '), na Yuri Zhirkov ( 68' )

    Katika mchezo mwingine Ureno ikiwa nyumbani imeitambia Ubelgiji baada ya kuichapa magoli 2-1 kwa magoli ya Cristiano Ronaldo na Luis Nani huku Romelo Lukaku akiifungia Ubelgiji goli la kufutia machozi akiunganisha pasi safi ya kaka yake Jordan Lukaku.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: UFARANSA YAICHAPA URUSI 4-2,URENO YAITAMBIA UBELGIJI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top