728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, March 23, 2016

    PIGO MAN UNITED!!BASTIAN SCHWEINSTEIGER NJE YA DIMBA MPAKA MSIMU UJAO

    Munich,Ujerumani.

    Klabu ya Manchester United imepata pigo baada ya kiungo wake Bastian
    Schweinsteiger kuripotiwa kuwa atakosa michezo yote iliyobakia ya ligi kuu nchini England baada ya kuumia goti.

    Schweinsteiger,31aliumia goti hilo siku ya jana jumanne wakati akifanya mazoezi na wachezaji wenzake katika kambi ya timu ya taifa ya Ujerumani inayotarajiwa kucheza michezo ya kirafiki ya kujipima nguvu dhidi ya England na Italia.

    Kwa mujibu wa vipimo vya MRI scan vilivyofanywa na daktari Hans-Wilhelm Müller-Wohlfahrt ni kuwa Schweinsteiger ameumiza vibaya goti lake na hivyo atakuwa nje ya dimba kwa kipindi kirefu na kuyaweka mashakani majaaliwa ya nyota huyo kucheza michuano ijayo ya Ulaya inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwezi Juni huko Ufaransa.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PIGO MAN UNITED!!BASTIAN SCHWEINSTEIGER NJE YA DIMBA MPAKA MSIMU UJAO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top