728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, March 29, 2016

    RWANDA YANG'ARA AFCON,YAIFUMIA MAURITIUS 5-0 AMAHORO

    Kigali,Rwanda.

    Rwanda imelipa kisasi cha kufungwa na Mauritius baada ya leo jioni kuichapa magoli 5-0 katika mchezo wa kundi H wa kufuzu michuano ya Afcon.

    Rwanda ikicheza katika dimba lake la nyumbani la Amahoro imepata magoli hayo kipitia kwa Dominique Nshuti aliyefunga mara mbili,Ernest Sugira,Fibna Omborenga na Jean Baptiste Muriganeza.Rwanda ilichapea goli 1-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa jumamosi.

    Kufuatia ushindi huo Rwanda imefikisha pointi sita na kushika nafasi ya pili ikiwa nyuma ya vinara Ghana wenye pointi nane.

    Kikosi cha Rwanda kilichoshuka dimbani leo:

    Ndayishimiye,Omborenga,
    Bayisenge,Rwatubyaye,
    Sibomana,Mukunzi,
    Nshimiyimana (Mugiraneza
    46'),Nshuti,Iranzi (Hakizimana 46'),Niyonzima (Rushenguziminega ),Sugira.




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RWANDA YANG'ARA AFCON,YAIFUMIA MAURITIUS 5-0 AMAHORO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top