728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, March 25, 2016

    NIGERIA YABANWA NYUMBANI NA MAFARAO WA MISRI

    Kaduna,Nigeria.

    Nigeria imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Misri katika mchezo mkali wa kundi G wa kusaka tiketi ya kushiriki michuano ya AFCON itakayopigwa Gabon mwakani.

    Nigeria ikicheza mbele ya mashabiki wake huko Ahmadu Bello,Kaduna ilifanikiwa kupata bao la kuongoza dakika ya 60 kupitia kwa Oghenekaro Etebo.

    Kuingia kwa bao hilo hakukuwavunja nguvu wageni Misri kwani dakika ya 90 winga Mohamed Salah aliwapatia bao la kusawazisha baada ya kumegewa pande zuri na Ramadan Sobhy. 

    Kufuatia matokeo hayo Misri bado iko kileleni mwa kundi G baada ya kufikisha pointi 7,nafasi ya pili inashikiliwa na Nigeria yenye pointi 5 huku Tanzania ikiwa na pointi 4 katika nafasi ya 3 huku Chad ikiwa haina pointi hata moja.

    Nigeria na Misri zitarudiana tena Machi 29 huko Alexandria,Misri.

    Vikosi

    Misri IX

    Ahmed El-Shennawy; Omar Gaber,Rami Rabia, Ahmed Hegazy, Hamada Tolba; Mohamed Elneny , Ibrahim Salah,Abdallah El-Said;Trezeguet, Koka,Mohamed Salah.

    Nigeria XI: Ikeme; Amuzie, Ambrose,Oboabona, Shehu Abdullahi; Mikel, Etebo,Iheanacho; Simon, Musa,Ighalo.





    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: NIGERIA YABANWA NYUMBANI NA MAFARAO WA MISRI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top