728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, March 26, 2016

    MAN UNITED SASA YAMGEUKIA MURILLO WA COLOMBIA

    Na Paul Manjale

    Milan,Italia.

    Manchester United imeripotiwa kujianda kumtwaa mlinzi mahiri wa Inter Milan ya Italia Mcolombia Jeison Murillo kwa ajili ya kuimarisha safu yake ya ulinzi ambayo msimu huu imekuwa ovyo.

    Kutoka gazeti la The Mirror la Uingereza taarifa zinadai kuwa Manchester United inamuona Murillo,23 kuwa ndiye mtu sahihi wa kuleta uimara katika safu yake ya ulinzi ambayo imekuwa ikimtegemea zaidi Chris Smalling.

    Murillo aliyefanya vyema mwaka jana akiwa na kikosi cha Colombia katika Copa America huko Chile na kutangazwa mchezaji bora kijana wa michuano hiyo anakadiriwa kuwa na thamani ya £15m.

    Msimu huu Murillo ameicheza Inter Milan jumla ya michezo 27 huku akiifungia mabao mawili.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAN UNITED SASA YAMGEUKIA MURILLO WA COLOMBIA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top