728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, March 28, 2016

    MANUEL PELLEGRINI APANIA KUBAKI ENGLAND BAADA YA KUACHANA NA MANCHESTER CITY

    Manchester,England.

    Kocha Manuel Pellegrini amedokeza kuwa atapendelea kubaki England hata baada ya kuachana na Manchester City mwishoni mwa msimu huu.

    Pellegrini,62 ambaye ataiacha Manchester City mikononi mwa Pep Guardiola hivi karibuni amedokeza kuwa England bado ni mahali sahihi kwa yeye kufanya kazi kama kocha.

    Licha ya kuhusishwa kujiunga na vilabu vya Valencia na Zenit St. Petersburg bado Pellegrini ameoneka kuwa mzito kuondoka England na amesisitiza kuwa akipata timu yoyote yenye project nzuri hatasita kujiunga nayo hata kama haishiriki michuano yoyote ile ya Ulaya.

    Akiongea na Telegraph Pellegrini amesema vilabu vya England vina mazingira mazuri ya kufanyia kazi,pesa nyingi na mipango mikubwa.Hata ukiwa kocha wa vilabu vidogo bado una nafasi ya kusajili wachezaji wazuri kwani pesa ipo.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MANUEL PELLEGRINI APANIA KUBAKI ENGLAND BAADA YA KUACHANA NA MANCHESTER CITY Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top