728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, July 06, 2015

    KWA ‘FIRST 11’ HII…SIMBA WATAIKOMA:


    WAKATI mchakato wa usajili wa Ligi Kuu Tanzania Bara ukiwa unaendelea, tayari Simba imeunda kikosi cha kwanza hatari ambacho kinaweza kuwa moto wa kuotea mbali dhidi ya timu pinzani.

    Tofauti na msimu uliopita
    , safari hii uongozi wa Simba umesajili kwa kuzingatia mahitaji na ubora wa wachezaji.

    Miongoni mwa usajili wa wachezaji wapya ambao huenda wakawa na msaada mkubwa Msimbazi, ni mshambuliaji Laudit Mavugo kutoka Vital’O ya Burundi ambaye rekodi yake ya kucheka na nyavu inatisha. 

    Msimu uliopita, Mavugo aliweka rekodi ya aina yake kwa kufunga mabao 31 ndani ya mechi 30, ambayo katika anga ya kimataifa, huwekwa na nyota wawili tu, Lionel Messi wa Bercelona na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KWA ‘FIRST 11’ HII…SIMBA WATAIKOMA: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top