728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, February 23, 2015

    CANNAVARO:WATANZANIA TUOMBEENI TUING'OE BDF XI

    Mbeya,Tanzania.

    Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub “Cannavaro”amewaomba Watanzania kuiombea timu yake ili ishinde mechi ya marudiano ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya wenyeji wao,BDF XI ya Botswana.
    Yanga watasafiri wikii hii kwa ajili ya mechi ya marudiano ya raundi kwanza. Katika mechi ya kwanza iliyofanyika Dar es Salaam takribani wiki moja iliyopita, Yanga, ikiwa chini ya kocha Mdachi, Hans Pluijm, walishinda 2-0.

    “Watanzania watuombee ili tushinde na kusonga
    hatua ya pili”, alisema Cannavaro,baada ya Yanga kuwafunga Mbeya City 3-1 katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara na kuongoza ligi wakiwa na pointi 31.
    “Mechi ya ugenini (away) mara nyingi huwa ni ngumu, tulishinda Dar es Salaam na tunahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili tusonge,Watanzania watuombee sisi na wenzetu Azam kwa sababu tunawakilisha nchi”, alisema Cannavaro.

    Yanga na mabingwa wa ligi kuu Tanzania Bara, Azam FC watakuwa na vibarua vya ugenini mwishoni mwa wiki.
    Azam watasafiri kwenda Khartoum, Sudan kucheza na El-Merreikh katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Katika mechi ya kwanza iliyochezwa Dar es Salaam,Azam ikiwa chini ya kocha Mcameroon,Joseph Omog walishinda 2-0.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CANNAVARO:WATANZANIA TUOMBEENI TUING'OE BDF XI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top