728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, February 13, 2015

    TANZANIA YAENDELEA KUSHUKA VIWANGO VYA SOKA

    Tanzania imeporomoka nafasi tatu kwa ubora wa viwango vya soka duniani vilivyotolewa na shirikisho la soka duniani (FIFA) hapo jana.Kwa mujibu wa shirikisho hilo Tanzania sasa ni ya 107 kutoka nafasi ya 104 iliyokuwa ikiishikiria mwezi uliopita.
                                                Tokeo la picha la taifa stars
    Katika nchi za ukanda wa CECAFA Rwanda ndiyo
    inaongoza ikiwa katika nafasi ya 72,Uganda 76,Ethiopia 102,Sudan 112,Kenya 116,Burundi 124,Sudan kusini 189 Eritrea 202,Somalia 204 na Djibout ikishika nafasi ya 206.
    Kwa upande mwingine mabingwa wapya wa Afrika Ivory Coast nyota njema imeendelea kuwawakia baada ya kupanda kwa nafsi nane katika orodha hiyo ya ubora wa soka na sasa inashika nafasi ya 20.Kidunia Ujerumani bado inashika nafasi ya kwanza ikifuatiwa na Argentina,Colombia,Ubelgiji na Uholanzi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TANZANIA YAENDELEA KUSHUKA VIWANGO VYA SOKA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top