728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, February 11, 2015

    MAJANGA ARSENAL:RAMSEY NJE MWEZI MMOJA,SANCHEZ MMHH!!

    London,England.

    Kiungo wa klabu ya Arsenal Aaron Ramsey ameendelea kuipa wakati mgumu klabu hiyo baada ya kuripotiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki nne tena.
     
    Ramsey 24 shujaa wa Arsenal wa msimu uliopiwa alitolewa
    dakika ya tisa tu ya mchezo wa jana jumanne wa ligi kuu dhidi ya Leceister City baada ya kuumia misuli.

    Ramsey ambaye alirejea uwanjani hivi karibuni baada ya kuwa nje kwa wiki sita kwa tatizo la misuli ataukosa mitanange ya hatua ya mtoano ya ligi ya mabingwa dhidi ya klabu ya Monaco ya Ufaransa.

    Habari njema kwa Arsenal ni kuwa nyota Alexis Sanchez ambaye pia aliumia na kulazimika kutolewa dakika ya 68 ameripotiwa kuwa katika hali nzuri japo huenda asishuke dimbani kuivaa Middlesbrough jumapili hii katika mchezo wa kombe la FA.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAJANGA ARSENAL:RAMSEY NJE MWEZI MMOJA,SANCHEZ MMHH!! Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top