728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, February 13, 2015

    RONALDINHO KUKIPIGA LIGI YA ANGOLA SIKU CHACHE ZIJAZO

     Luanda,Angola.

    Kiungo mshambuliaji wa zamani wa vilabu vya Barcelona,Ac Milan,Paris Saint Germain na timu ya taifa ya Brazil Ronaldinho 34 ameripotiwa kuwa karibu kutua katika klabu ya Kabuscorp inayoshiriki ligi ya Angola.
     
                                   Queretaro's Ronaldinho gestures during a Copa MX soccer match against Tigres at the Corregidora stadium in Queretaro (Reuters)
    Ronaldinho ambaye kwa sasa anakipiga na klabu ya Queretaro
    ya Mexico iliyomsajili kwa uhamisho wa miaka miwili na nusu mwezi septemba mwaka jana yuko katika hatua nzuri ya mazungumzo ya kutua Angola kupitia kwa wakala wake.

    Akipasha habari hizo raisi wa klabu ya Kabscorp bwana Benedicto Kangamba amesema "Tuko katika mazungumzo na wakala wa mchezaji Ronaldinho kwa ajili ya kumsajili nyota huyo mshindi wa kombe la dunia.Matumaini ni makubwa kuwa tutamsajili"

    "Tukiwa na mchezaji kama Ronaldinho naamini tunaweza kushinda ubingwa wa michuano ya kombe la ligi ya mabingwa Afrika na kisha kupata nafasi ya kucheza michuano ya vilabu bingwa duniani ambapo tutapimana ubavu na vilabu vya Ulaya"

    Alimaliza raisi huyo ambaye klabu yake mwaka 2012 iliweka rekodi ya kumsajili nyota mwingine wa Brazil Rivaldo Boba Ferreirra.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RONALDINHO KUKIPIGA LIGI YA ANGOLA SIKU CHACHE ZIJAZO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top