728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, October 30, 2014

    NYOTA WANNE YANGA KUIKOSA KAGERA LIGI KUU BARA

    WACHEZAJI wanne wa kikosi cha Yanga
    wataikosa mechi ya wikiendi hii dhidi ya
    Kagera Sugar baada ya kukumbwa na
    matatizo mbalimbali.

    Daktari wa Yanga, Juma Sufiani,
    amewataja wanne hao kuwa ni mabeki;
    Nadir Haroub ‘Cannavaro na Kelvin
    Yondani wanaosumbuliwa na malaria,
    winga machachari Simon Msuva
    anayesumbuliwa na mgongo wakati
    Hussein Javu yeye ameumia goti.
    Sufiani alisema kuwa Msuva aliumia
    mazoezini wakati Javu aliumia goti
    kwenye mechi dhidi ya Stand United
    wikiendi iliyopita.

    “Wote tumewaandikia mapumziko ya wiki
    nzima ili waweze kupona kabisa, si
    matatizo makubwa, lakini ni vyema
    wakapumzika. Javu atafanyiwa vipimo
    baada ya kurejea Dar ili kubaini ukubwa
    wa tatizo lake,” alisema Sufiani.
    Katika hatua nyingine, beki wa kulia wa
    Yanga, Oscar Joshua, ameweka wazi siri
    ya safu yao ya ulinzi kufanya vizuri
    akisema ni namna wanavyonolewa na
    kocha Marcio Maximo.

    Alisema: “Ubora wa safu yetu kusema
    kweli, siri ni kujituma wenyewe, lakini
    pili ni kufuata maelekezo ya kocha wetu
    Maximo kwani mfumo anaotufundisha wa
    namna ya kuzuia, kuijenga ngome yetu
    lazima ufanye kazi.

    “Kocha amekuwa akitupa mbinu ambazo
    ni ngumu kwa wapinzani kutupita. Kazi
    hii iliimarishwa mara baada ya mechi ile
    tuliyofungwa na Mtibwa. Kwa staili hii
    tunayocheza, hata kama mimi sitakuwepo
    au mwingine yeyote, atakayeingia
    akicheza kwa maelekezo, ni ngumu
    kufungwa,”alisema Oscar.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: NYOTA WANNE YANGA KUIKOSA KAGERA LIGI KUU BARA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top