728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 03, 2014

    KAZI IPO LIGI KUU BARA:MBEYA CITY,COASTAL ZASHIKANA UCHAWI

    HALI ya mambo inaonekana siyo shwari baina ya timu mbili kutoka mkoani Mbeya na Tanga, ambapo imani za kishirikina zimetajwa kuhusika na sasa kila upande umeamua kukimbilia kushitaki kwa Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF).

    Coastal Union walifungwa bao 1-0 na Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, lakini baada ya mchezo huo Coastal wakaibuka na kusema wenyeji wao hao waliwafanyia vitendo vingi vinavyohusiana na imani za kishirikina, Mbeya City kusikia hivyo, wakakanusha vikali na kusema hawako
    tayari kudhalilishwa.

    Kiongozi wa msafara na mjumbe wa Kamati ya Utendaji  ya Coastal, Albert Clement Peter, ameliambia gazeti hili kuwa vitendo walivyofanyiwa na Mbeya City havikuwa vya kiuungwana hata kidogo hivyo wamepeleka barua yao TFF.

    “Walianza kufanyiwa usiku katika hoteli tuliyofikia ya…(anaitaja), hata chumba cha kubadilishia nguo uwanjani kilipigwa rangi na tukashindwa kuingia. Tumeshapeleka barua ya kushitaki TFF,” alisema Albert.
    Upande wa Mbeya City kupitia Ofisa Habari, Dismas Ten alisema kipigo kiliwachanganya wapinzani wao na ndiyo maana wanaanza kusingizia masuala ya ushirikina jambo ambalo si la kweli.“Suala hili tutalipeleka TFF, hicho wanachokisema ni udhalilishaji wa wazi,” alisema Ten.

    Habari kwa msaada wa Global publishers
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KAZI IPO LIGI KUU BARA:MBEYA CITY,COASTAL ZASHIKANA UCHAWI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top