728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 31, 2014

    LIGI KUU ENGLAND KUENDELEA KESHO JUMAMOSI

    Kitimtim cha ligi kuu ya England kitaendelea
    tena kesho wakati ambapo mashabiki wa soka
    nchini humo na duniani kote watapata nafasi
    ya kuzishuhudia timu zao zikitafuta pointi tatu
    muhimu.

    Newcastle Utd wataikaribisha Liverpool katika
    mchezo ambao utarushwa moja kwa moja
    kupitia idhaa ya Kiswahili ya BBC majira ya
    saa tisa unusu kwa saa za Afrika Mashariki.

    Arsenal wao wataikaribisha Burnley, huku
    Chelsea nayo wakiialika QPR. Everton
    watakuwa nyumbani kucheza Swansea City.
    Hull City wataikabili Southampton. Michezo
    mingine ni itakayochezwa siku hiyo ya kesho
    ni kati ya Leicester City watakapo kwaana na
    West Brom, Huku Stoke City watakapoikabili
    West Ham utd.

    Siku ya jumapili ni mpambano wa kukata na
    shoka ambapo Manchester United
    wataavaana na Manchester City mechi
    ambayo pia itatangazwa moja kwa moja na
    Idhaa ya Kiswahili ya BBC ,huku Tottenham
    watakapokwaana na Aston villa.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIGI KUU ENGLAND KUENDELEA KESHO JUMAMOSI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top