728x90 AdSpace

Thursday, October 09, 2014

BENZEMA AILILIA BARCELONA



Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid Mfaransa Karim Benzema anaamini kuwa lazima klabu ya Barcelona ibaki La Liga hata kama jimbo la Catalunya inakotoka klabu hiyo litafanikiwa kutimiza ndoto yake ya kutaka kujitenga na Hispania na kuwa taifa linalojitegemea.

 
Wakati mbichi na mbivu za sakata hilo lililodumu kwa kipindi kirefu sasa likisubiri Novemba 22 mwaka huu kujua kama Catalunya itaachiwa na kuwa taifa huru tayari raisi wa chama cha soka cha Hispania (LFP) Javier Tebas ameshatanabaisha kuwa mabingwa hao wa mara 22 wa taji la La Liga na wapinzani wao wa mji mmoja klabu ya Espanyol hawataruhusiwa
kushiriki tena ligi hiyo mara jimbo hilo litakapokuwa limejitenga.


Lakini Benzema  anahisi kuwa ni muhimu Barcelona ikaendelea kuwepo La Liga amesema

“Tunaihitaji Barcelona ibaki kwenye ligi.Hakuna kitu kikubwa kama kuiona Barcelona ikiumana na Madrid”


“Kama wanataka kujiondoa La Liga hilo litakuwa ni tatizo,napenda mambo yabaki kama yalivyo na Barcelona tuendelee kuwa nao”Alimaliza Benzema

Taarifa zilizoibuka jana zinasema kuwa tayari maafisa wa klabu ya Barcelona wameshaanza kufanya mpango wa kuihamishia klabu hiyo katika ligi ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1 kama hawatotambuliwa baada ya jimbo lao kujitenga.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: BENZEMA AILILIA BARCELONA Rating: 5 Reviewed By: Unknown