728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 17, 2014

    YANGA YABADILI REFA MECHI VS SIMBA

    Kamati ya Waamuzi nchini imemuondoa refa
    msaidizi namba moja, Ferdinand Chacha
    kuchezesha mechi ya watani wa jadi, Yanga
    na Simba, na nafasi yake sasa inachukuliwa
    na Samuel Mpenzu kutoka Arusha ambaye
    atasaidiana na John Kanyenye kwenye
    mchezo huo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania
    Bara ambao mwamuzi wa kati atakuwa Israel
    Nkongo.

    Hata hivyo, mabadiliko hayo yaliyofanywa na
    kamati hiyo yalichelewa kufika katika
    sekretarieti ya Shirikisho la Soka nchini (TFF),
    ambayo juzi ilimtangaza Chacha na Kanyenye
    wa Mbeya kuwa watamsaidia Nkongo katika
    mechi hiyo namba 27 itakayopigwa Uwanja
    wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi
    Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana jijini
    jana kutoka kwa chanzo chetu muhimu ndani
    ya kamati hiyo, zinaeleza maamuzi ya
    kumuondoa mwamuzi huyo yametokana na
    'shinikizo' kutoka kwa viongozi wa klabu ya
    Yanga ya jijini ambao wanadaiwa kumkataa
    Chacha ambaye pia aliwachezesha katika
    mechi yao ya kwanza dhidi ya Mtibwa Sugar
    iliyofanyika mkoani Morogoro.

    Taarifa zaidi zinadai kwamba Yanga
    iliwasilisha maombi ya kumkataa Chacha kwa
    kamati na hatimaye mwamuzi huyo mwenye
    beji inayotambuliwa na Shirikisho la Soka
    duniani (Fifa) kuondolewa.
    Habari zaidi kutoka kwa chanzo chetu
    ziliendelea kueleza kwamba baada ya Yanga
    kumkataa, mwamuzi huyo alitakiwa kuandika
    barua ya kuomba aondolewe kuchezesha
    mechi hiyo lakini Chacha hakuwa tayari
    kufanya hivyo.

    Hata hivyo, kiongozi mmoja wa juu wa TFF
    anadaiwa naye kushiriki katika mabadiliko
    hayo ya kumuengua Chacha kwa kumueleza
    kwamba asilazimishe kuuchezesha mchezo
    huo wa watani wa jadi kwa sababu unaweza
    kuharibu rekodi yake.

    Mwenyekiti wa Kamati wa Waamuzi nchini,
    Salum Chama, aliliambia gazeti hili kwa njia
    ya simu kuwa ni kweli kamati hiyo imefanya
    mabadiliko lakini hayatokani na shinikizo
    lolote.

    Chama alisema sababu kubwa ni kubaini kuwa
    Chacha alichezesha mechi kati ya Mtibwa
    Sugar na Yanga ambayo ilimalizika kwa kikosi
    cha Mbrazil Marcio Maximo, kuchapwa mabao
    2-0.

    "Kamati ndiyo yenye maamuzi ya kupanga na
    kubadilisha mwamuzi, tumepangua kwa
    sababu tumeona si vyema mwamuzi mmoja
    kuambatana na timu moja ndani ya muda
    mfupi, hakuna sababu nyingine kama
    ulivyoniuliza," alisema Chama kwa kifupi.

    Lakini kwa upande wa Mkurugenzi wa
    Mashindano wa TFF, Boniface Wambura,
    alisema shirikisho halihusiki na mabadiliko
    hayo.
    Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto,
    hakuwa tayari kuelezea madai hayo.

    Rais wa Simba, Evance Aveva, alisema "yote
    sawa, kama wameamua kumbadilisha sisi
    kwetu mpira ni dakika 90".

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: YANGA YABADILI REFA MECHI VS SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top