728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 01, 2014

    TOTTI AWA MCHEZAJI KIKONGWE ZAIDI KUFUNGA GOLI LIGI YA MABINGWA



    Mshambuliaji mkongwe wa klabu ya Roma ya Italia Francesco Totti licha ya kuisaidia klabu yake kuondoka na pointi moja (1) dhidi ya klabu ya Manchester City katika dimba la Etihad jijini Manchester usiku wa jana katika michuano ya ligi ya mabingwa wa Ulaya pia aliweka rekodi
    ya kuwa mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kuwahi kufungwa goli katika michuano hiyo.


    Totti ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 38 na siku 3 alifunga goli hilo dakika ya 23 ya mchezo huo na kusawazisha goli la mapema la mshambulaji Sergio Aguero na hatimaye kuvunja rekodi hiyo iliyokuwa ikishikiriwa na nyota wa zamani wa klabu ya Manchester United Ryan Giggs aliyefunga akiwa na miaka 37 na siku 290 dhidi ya klabu ya SL Benfica mwaka 2011/12.


    Orodha kamili ya nyota wenye umri mkubwa zaidi kuwahi kufunga goli katika michuano ya ligi ya mabingwa hii hapa…..

    Francesco Totti – 38 years 3 days – Manchester City v AS Roma, 30/09/14

    Ryan Giggs – 37 years 290 days – SL Benfica v Manchester United FC, 14/09/11

    Filippo Inzaghi – 37 years 87 days – AS Milan v Real Madrid CF, 03/11/10

    Javier Zanetti – 37 years 72 days – FC Internazionale Milano v Tottenham Hotspur FC, 20/10/10

    Laurent Blanc – 36 years 339 days – Olympiacos FC v Manchester United FC, 23/10/02

    Paolo Maldini – 36 years 334 days – Liverpool FC v AC Milan, 25/05/05

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TOTTI AWA MCHEZAJI KIKONGWE ZAIDI KUFUNGA GOLI LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top