728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, October 09, 2014

    SANCHEZ:WENGER NATAKA KUCHEZA DAKIKA 90

    Nyota wa klabu ya Arsenal Alexis Sanchez amekiri kuwa anachukizwa mno na kitendo cha kuwekwa benchi na kocha Arsene Wenger na kuongeza kuwa nafasi aipendayo ni wingi ya kushoto.


    Tangu atue klabuni hapo tayari Sanchez ameshatumiwa katika nafasi zote za ushambuliaji,wingi zote kulia na kushoto pamoja na ushambuliaji wa kati.Akifanya mahojiano na tovuti ya klabu hiyo Sanchez mwenye magoli matano mpaka sasa amekiri kukasirishwa kutolewa katika mchezo dhidi ya Galatasaray pamoja na kuanzia benchi katika michezo miwili ya ligi dhidi ya Aston Villa na Tottenham.
    Amesema 

    “Naweza kukimbia na kuingia
    ndani vizuri nikitokea kushoto lakini nafasi yoyote ile ni nzuri kwangu ilimradi nacheza mpira kuliko kukaa benchi”
    “Ukinitoa mchezoni ni sawa na kuniibia mpira miguuni mwangu” 
    “Nataka kushinda kila kitu,ukitazama aina ya kocha tuliyenaye,wachezaji waliopo na njaa waliyonayo,tunaweza kushinda karibu kila kitu”

    Wakati huo huo nyota huyo amesema kuwa ligi ya England ni ngumu kuliko ile ya Hispania lakini inavutia.
    Amesema  

    “Ukilinganisha na ligi nyingine ambazo nimewahi kucheza La Liga na Seria A,Epl ni ngumu sana lakini nimetokea kuipenda mno”
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SANCHEZ:WENGER NATAKA KUCHEZA DAKIKA 90 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top