728x90 AdSpace

Wednesday, October 08, 2014

LIVERPOOL YAMGEUKIA TIOTE



Taarifa kutoka ndani ya klabu ya Liverpool zinasema klabu hiyo iko mbioni kumnasa kiungo wa klabu ya Newcastle Cheick Tiote kwa dau la paundi milioni 15.5 hapo mwezi januari.



Liverpool inaonekana kuipiku Arsenal na kukalia kiti cha uongozi wa mbio za kumnasa kiungo huyo asiye na masihara pindi awapo dimbani.Tiote hivi karibuni ameiambia klabu yake kuwa
muda wake wa kutafuta changamoto mpya umefika hivyo Newcastle iheshimu maamuzi hayo.


Inasemekana Newcastle inataka angalau kiasi cha paundi milioni 20 ili iweze kumuachia kiungo huyo iliyemsajili miaka minne iliyopita toka klabu ya FC Twende ya Uholanzi.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: LIVERPOOL YAMGEUKIA TIOTE Rating: 5 Reviewed By: Unknown