728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, October 30, 2014

    MASHABIKI LIVERPOOL WARUDISHA JEZI ZA BALOTELLI

    HII ni kali. Mashabiki wa Liverpool
    wameripotiwa kurudisha jezi za Mario
    Balotelli walizonunua baada ya staa huyo
    kujiunga na timu hiyo ili wapewe za
    mastaa wao makini baada ya Mtaliano
    huyo kuchemsha.

    Mashabiki kadhaa walionekana
    wakipanga mstari na jezi zao zilizokuwa
    zimeandika ‘Balotelli 45’ mgongoni kuvua
    ili kupewa nyingine za mastraika
    waliofanya vizuri kwenye kikosi hicho
    kama Rush, Fowler na Owen.
    Tukio hilo lilifanyika Jumamosi iliyopita
    kwenye mechi dhidi ya Hull City baada ya
    mashabiki hao kukerwa na kitendo cha
    Balotelli kubadilishana jezi na Pepe wa
    Real Madrid wakati wa mapumziko
    kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
    iliyomalizika kwa Liverpool kuchapwa
    mabao 3-0.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MASHABIKI LIVERPOOL WARUDISHA JEZI ZA BALOTELLI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top