728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, October 09, 2014

    SOL CAMPBELL:MWONDOENI GARY NEVILLE MNIWEKE MIMI



    Gary Neville anapaswa kuondelewa kuwa kocha wa England na nafasi hiyo akapewa Sol Campbell,hiyo ni kwa mujibu wa Campbell mwenyewe.

     
    Campbell ambaye ameichezea timu ya taifa ya England michezo 73 na kufunga goli moja kati ya mwaka 1996 na 2007 anaona Neville ambaye ameichezea timu hiyo michezo 85 bila ya kufunga goli lolote kati ya mwaka 1995 mpaka 2007 anapaswa kuondolewa katika nafasi yake ya ukocha msaidizi katika timu ya taifa ya England.Campbell na Neville wameitumikia klabu hiyo kwa miaka 11.

    Akijibu swali aliloulizwa na shabiki mmoja wa soka katika tamasha la Cheltenham Literature Festival ni nini kifanyike ili timu hiyo iache kufungwa magoli ya ajabu ajabu (mengi) Campbell alijibu



    “Mwondoeni Gary Neville na nafasi hiyo mnipe mimi kwa kuwa nina sifa zote.Najua nini cha kufanya ili vijana wafanye vizuri

    Mpaka sasa England hawajaruhusu goli lolote lile katika michezo yake minne tangu ilipoondolewa kwa aibu katika fainali za kombe la dunia kwa kupokea vichapo toka kwa Italia na Uruguayi.

    Wakati Neville akiwa na leseni A na B inayotambuliwa na UEFA,Campbell aliendelea kujinadi 

    “Kwa sasa nafanya mafunzo ya ukocha yanayotambuliwa na chama cha soka cha Walace.Niko katika mwaka wa mwisho wa mafunzo.Kama sitopata kazi kufundisha hapa ndani ya miaka michache nitaangalia sehemu nyingine pia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SOL CAMPBELL:MWONDOENI GARY NEVILLE MNIWEKE MIMI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top