728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 10, 2014

    JE,NI KWELI SAN MARINO NDIYO TIMU KIBONDE ZAIDI DUNIANI?

    Kabla ya mchezo wa jana alhamisi wa kundi D wa kusaka tiketi ya kushiriki michuano ijayo ya Ulaya (Euro 2016) kati ya England na San Marino swali kubwa ukiachana na pointi tatu(3) muhimul ilikuwa ni magoli mangapi vijana wa Roy Hodgson wangeifunga San Marino ambayo kwa takwimu na rekodi mbali mbalimbali pengine ndiyo timu dhaifu zaidi katika uso wa dunia.

     
    Historia ya timu hii inayoundwa na wauza mitumba,wafanyakazi wa viwandani na wamiliki wa baa inaanzia mwaka 1990 ambapo ilishuka dimbani kwa mara ya kwanza kucheza kama timu kamili ya taifa katika mchezo unaotambuliwa rasmi na mashirikisho ya soka,tangu hapo wamekuwa wakiweka rekodi za kuzivunja wenyewe.


    YAFUATAYO NI MAMBO KUMI USIYOYAJUA KUHUSU SAN MARINO

    1.  San Marino wameshinda mchezo mmoja (1) tu katika historia tena kwa kuwafunga vibonde wengine Liechtenstein 1-0 katika mchezo wa kirafiki hii ikiwa ni mwaka 2004.

    2.    Katika orodha ya viwango vya ubora vya FIFA,San Marino wanaburuza mkia wakifungana na taifa la Bhutan katika nafasi ya 208.


    3.      Katika michezo mitano waliyokutana na England wamebamizwa jumla ya magoli 31 huku wao wakifanikiwa kufunga goli 1 tu.(San Marino walifungwa magoli 13 na England katika michezo miwili tu
    ya kusaka tiketi ya kushiriki kombe la dunia nchini Brazil)


    4.      Ndugu wawili mapacha Aldo na Davide Simoncini waliweka rekodi ya kujifunga katika mchezo ulioisha kwa San Marino kubugizwa magoli 6-0 na Sweden hii ikiwa ni mwaka 2010.

    5.      Taifa la San Marino lina wakazi wapatao 32,000 tu,ambao ni sawa na nusu ya  idadi ya watazamaji walijitokea katika mchezo wa jana pale Wembley.

    6.      Ligi ya San Marino inaitwa Campionato Sammarinese di Calcio ambayo wao huifananisha na ligi kuu ya England,katika vilabu vyote hivyo hakuna hata kimoja chenye uwanja wake hivyo basi kimoja kati ya viwanja vitano huchagulia kiholela kwa ajili ya ligi kuchezwa.
    Uwanja wa taifa wa San Marino unaochukua watu 6,664


    7.      Katika michezo rasmi ambayo San Marino wamecheza wamefanikiwa kufunga jumla ya magoli 20 tu huku wao wakibugizwa magoli 536.


    8.      San Marino bado inahaha kuboresha kiwango chake katika miaka ya karibuni toka mwaka 2008 mpaka sasa katika michezo 30 ya kusaka tiketi za kombe la dunia na euro  wamefanikiwa kufunga magoli 2 tu na kufungwa 159.

    9.      Waliweka rekodi mbaya zaidi mwaka 2006 katika mchezo wa kusaka tiketi ya kufuzu michuano ya Ulaya (Euro) baada ya kukubali kichapo cha magoli 13-0 dhidi ya Ujerumani.
     



    10.  Goli la Davide Gaulteris la sekunde ya 7 dhidi ya England mwaka 1993 ndilo linabaki kuwa ni goli la mapema zaidi katika michezo ya kufuzu kuelekea kombe la dunia,katika mchezo huo San Marino walifungwa magoli 7-1.


    MATOKEO YA JANA
    England 5 – 0 San Marino (Wayne Rooney 1,Phil Jagielka 1,Danny Welbeck 1,Della Valle na Andros Townsend 1)
    Uwanja: Wembley 55,990

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: JE,NI KWELI SAN MARINO NDIYO TIMU KIBONDE ZAIDI DUNIANI? Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top