728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 08, 2014

    CECH KUTIMKA CHELSEA BENCHI LIKIENDELEA



    Mlinda mlango aliyepoteza namba katika kikosi cha kwanza cha klabu ya Chelsea Peter Cech hatimaye amevunja ukimya na kusema kuwa atatimka klabuni hapo ikiwa ataendelea kusota benchi.

     
    Cech  (32) ambaye amepoteza namba tangu kuwasili kwa mlinda mlango Thibaut Courtois ameshaichezea klabu hiyo jumla ya michezo
    472 na kutwaa mataji kadhaa lakini msimu huu amefanikiwa kucheza jumla ya michezo miwili tu.


    Cech amesema “Bado sijaongea na yoyote,lakini nafikiri wananifahamu vizuri kiasi cha kugundua kuwa hali ni tofauti na nilivyofikiri”

    “Euro 2016 inakuja na nikifikiria hatima yangu timu ya taifa nadhani sina sababu ya kuendelea kukaa benchi”

    “Kama hali hii haitapata jibu,nitatafuta mwenyewe njia ya kutatua “
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CECH KUTIMKA CHELSEA BENCHI LIKIENDELEA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top