728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, October 02, 2014

    MONK: KUITWA KWA SHELVEY NI MWANZO WA MAMBO MAZURI TOKA SWANSEA



    Kocha mkuu wa klabu ya Swansea City Garry Monk amesifia uteuzi wa kiungo wake aliye katika kiwango kizuri Jonjo Shelvey katika kikosi cha timu ya taifa ya England kilichotajwa leo hii na kocha Roy Hodgson kwa ajili ya michezo miwili ya kusaka tiketi ya kufuzu kucheza michuano ijayo ya Ulaya,Euro 2016 dhidi ya San Marino na Estonia.



    Monk amesema kuitwa kwa nyota huyo kwa mara nyingine tena katika kikosi hicho baada ya kufanya hivyo mwaka 2012 kutafungua  zaidi milango kwa nyota wakekutambulika kimataifa.Monk amesema


     “Ni habari nzuri kwa Shelvey na klabu kwa ujumla.Tuna wachezaji wengi wa kimataifa hapa lakini kwa upande wa England tumekuwa hatuna bahati hiyo. Hivyo kwa uteuzi huo nadhani hii ni nafasi nzuri hata kwa wengine pia kuanza kutazamwa”  


    “Watu wanataka England icheze mpira wa pasi na kushambulia,hii ni aina ya mpira ambao Swansea tumekuwa tukiucheza kwa kipindi kirefu sasa.Akiongezeka mwingine katika kikosi cha Hodgson tutashuhudia mpira mzuri sana”.

    Mbali ya Shelvey pia Swansea imetoa wachezaj kadhaa katika timu mbalimbali za taifa kama vile Ki Sung Yueng (Korea),Gylfi Sigurdsson ( Iceland)na Wilfred Bony (Ivory Coast)

    Kikosi kamili kilichotajwa na Roy Hodgson ni kama ifuatavyo…..


    GOALKEEPERS
    Fraser Forster (Southampton), Ben Foster (West Bromwich Albion), Joe Hart (Manchester City)

    DEFENDERS
    Leighton Baines (Everton), Gary Cahill (Chelsea), Nathaniel Clyne (Southampton), Kieran Gibbs (Arsenal), Phil Jagielka (Everton), John Stones (Everton)

    MIDFIELDERS
    Fabian Delph (Aston Villa), Jordan Henderson (Liverpool), Adam Lallana (Liverpool), James Milner (Manchester City), Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Jonjo Shelvey (Swansea City), Raheem Sterling (Liverpool), Andros Townsend (Tottenham Hotspur), Jack Wilshere (Arsenal)

    FORWARDS
    Rickie Lambert (Liverpool), Wayne Rooney (Manchester United), Daniel Welbeck (Arsenal)




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MONK: KUITWA KWA SHELVEY NI MWANZO WA MAMBO MAZURI TOKA SWANSEA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top