728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 17, 2014

    BEKI YANGA ANUNUA VIATU VIPYA KISA OKWI/MESSI

    Wakati kikosi cha Yanga
    kikitarajiwa kushuka
    uwanjani kesho Jumamosi
    kupambana na wapinzani wao
    wa jadi, Simba, beki wa
    kushoto wa timu hiyo, Oscar
    Joshua, amenunua viatu
    vipya kwa ajili kukabiliana
    na washambuliaji wa Simba,
    Emmanuel Okwi na Ramadhan
    Singano ‘Messi’.

    Joshua, mwenyeji wa Mwanza,
    amefikia hatua hiyo
    kuhakikisha anawadhibiti
    vilivyo wachezaji hao ambao
    wanasifika kwa kuwa na kasi
    kali pindi wanapokuwa
    uwanjani.

    Mchezaji wa Yanga ambaye
    amesema si ishu kubwa yeye
    kutajwa, amesema Joshua
    amewapania vilivyo
    wachezaji hao ambao
    wamekuwa chachu ya mabao ya
    Simba, kuhakikisha
    hawatengenezi nafasi yoyote
    ya kufunga katika mechi
    hiyo.

    “Unajua hivi sasa kuna hali
    kama ya mvuamvua, hivyo
    ameamua kutafuta viatu
    vipya ambavyo vitamsaidia
    kutoteleza kila wakati
    pindi atakapokuwa
    akikabiliana na wachezaji
    hao.

    “Okwi na Messi wanajulikana
    kwa kuwa na chenga za
    maudhi, hivyo kama mchezaji
    akiwa na viatu ambavyo meno
    yake siyo mazuri, wanaweza
    kumuaibisha na hilo ndilo
    lililomfanya Oscar afanye
    hivyo,” kilisema chanzo
    hicho cha habari.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BEKI YANGA ANUNUA VIATU VIPYA KISA OKWI/MESSI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top