728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 08, 2014

    WENGER KUMWAGA NOTI JANUARI



    Kocha mkuu wa klabu ya Arsenal Mfaransa Arsene Wenger anafikiria kutumia kiasi cha paundi milioni 60 za Uingereza kwa ajili ya kukiimarisha kikosi chake mwezi januari mwakani.


    Wenger ambaye tayari ametumia zaidi ya paundi milioni 70 wakati wa kipindi cha majira ya joto kusajili nyota kama Alexis Sanchez,Calum Chambers,Danny Welbeck,Mathieu Debuchy na mlinda mlango David Ospina anahusishwa kuwawinda nyota kama
    Sami Khedira,Julian Draxler na Mbrazil Anderson Talisca.

    Kwa mujibu vya vyombo mbalimbali vya habari vya Hispania taarifa zinasema tayari Arsenal imeshakubaliana kila kitu na kiungo wa Real Madrid Sami Khedira  (27) ikiwemo mshahara wa paundi 100,000 kwa wiki kinachosubiriwa kwa sasa ni makubaliano ya ada ya uhamisho baina ya vilabu hivyo viwili.

    Ada ya usajili wa Khedira huenda ikiwa chini ya paundi milioni 10 kutokana na nyota huyo kuwa katika kipindi cha mwisho kabisa cha mkataba wake katika klabu ya Real Madrid.

    Pia klabu ya Arsenal imejiunga katika mbio za kumsajili mshambuliaji raia wa Brazil anayekipiga katika klabu ya Benfica ya Ureno Anderson Talisca (20).Talsica amevuta hisia za makocha wengi Ulaya baada ya kuanza msimu wa ligi ya Ureno kwa style ya aina yake baada ya kuifungia Benfica magoli 6 katika michezo 7 na kuifanya klabu hiyo iendelee kuongoza huku ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja

    .
    Talisca ambaye alijiunga na Benfica mwezi Julai kwa ada ya paundi milioni 3 akitokea klabu ya Bahia ya nyumbani kwao Brazil inasemekana katika mkataba wake kuna kipengere kinachomruhusu kuhama kwa ada ya paundi milioni 18.Mbali ya Arsena vilabu vingine vinavyomtolea macho kinda huyo ni Liverpool,Chelsea na Manchester United.

    Taarifa nyingine zinasema kuwa kocha Arsene Wenger anafikiria tena kufufua ndoto za kumfukuzia kiungo wa klabu ya Shalke 04 ya Ujerumani Julien Draxler baada ya kumshindwa kumnasa hapo mwezi januari kwa kile kinachodaiwa dau kubwa la usajili lililotakiwa na klabu yake la paundi milioni 37.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WENGER KUMWAGA NOTI JANUARI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top