728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, October 28, 2014

    MUUAJI WA SENZO MEYIWA BADO KITENDAWILI

    Polisi nchini Africa Kusini wameanzisha msako
    mkali dhidi ya mtu aliyempiga risasi na
    kumuua kipa na kapteni wa timu ya taifa hilo
    Senzo Meyiwa.

    Ili kufanikisha na kuufanya uchunguzi wao
    uwe rahisi na wa haraka,polisi hao wametoa
    zawadi nono ya randi 250,000 sawa na dola
    za kimarekani 14,000; hadi $23,000 kwa
    yeyote atakayefanikisha taarifa za kukamatwa
    kwa mtu huyo,ambaye anaongeza namba ya
    matukio ya uhalifu yaliyokithiri nchini humo.

    Meyiwa, amekufa akiwa na umri wa miaka 27,
    inaarifiwa kuwa alipigwa risasi na kuuawa na
    mtu aliyeingia nyumbani kwa mpenzi wake na
    kutekeleza mauaji hayo.
    Rais wa taifa hilo Jacob Zuma ametuma
    salamu za rambi rambi na kutoa ujumbe
    kwamba maneno hayatoshi kuonesha
    mshtuko wa taifa letu kwa kuuawa kwa
    Meyiwa.

    Polisi wametoa taarifa kuwa si mtu mmoja
    bali walikua wanaume wawili waloingia
    nyumbani na mmoja alibaki nje ya nyumba
    hiyo huko kwenye kitongoji cha
    Vosloorus,jijini kusini mwa Johannesburg,na
    walipoingia wakadai Meyiwa .
    Rais Jacob Zuma amesema kwamba taifa lake
    linaomboleza kifo cha mchezaji nguli na
    mchanga na kiongozi wa timu ya taifa
    ambaye maisha yake yamepokwa angali
    mdogo na katika kilele cha mafanikio yake ,
    na maneno pekee hayatoshi kuelezea hasara
    waliyopata.

    Vituo vya redio na runinga vina pokea ujumbe
    wa pole kwa kifo cha Meyiwa .
    Tukio hilo la kupigwa risasi kwa Meyiwa
    kunaonesha taswira ya matumizi mabaya ya
    silaha nchini Africa Kusini, ikiwa ni siku
    chache tu kesi ya mwanariadha Osca
    Pistorious iliporindima nchini humo na
    kutolewa maamuzi ambayo hayajawaridhisha
    walio wengi nchini humo.
    Taifa hilo linajiuliza maswali lenyewe juu ya
    kuongezeka kwa matukio ya uhalifu nchini
    humo,na wanaouawa ni watu wenye vipaji vya
    kipekee kama miaka saba iliyopita aliuawa
    nguli wa muziki wa reggae Lucky Dube .

    Jambo kubwa na la msingi kwa sasa dunia
    imewageukia wanamgambo wa
    kiislamu,wakati kuna uhalifu duniani kote.
    Meyiwa alizaliwa mnamo tarehe 24
    September ,mwaka 1987
    Alikuwa ni kipa wa timu kutoka Johannesburg
    ya Orlando Pirates
    Alijiunga na timu ya taifa hilo mwaka 2013
    Mwaka uliofuata alichaguliwa kuwa kapteni
    wa timu ya taifa.

    Na kuilete nchi yake vikombe saba vya
    ushindi alikuwa na mpenzi ambaye ni
    muigizaji Kelly Khumalo ambaye alipata naye
    mototo mmoja naye.

    Meyiwa anatajwa kuwa kipa bora barani
    Africa .

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MUUAJI WA SENZO MEYIWA BADO KITENDAWILI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top