728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 10, 2014

    SCHOLES:WILSHERE NA STERLING WARUDI KIKOSI CHA VIJANA U21



    Nyota wa zamani wa kikosi cha timu ya taifa ya England Paul Scholes ambaye kwa sasa ni mchambuzi wa soka amesema kiungo  wa Arsenal Jack Wilshere na winga wa Liverpool Raheem Sterling wanapaswa  kuwemo katika kikosi cha vijana cha nchi hiyo kitakachoshiriki michuano ijayo ya Ulaya hapo mwakani.
     

    Kikosi hicho cha vijana (U21) ambacho mpaka sasa kimeshinda michezo yake 9 kati ya 10 usiku wa leo kitajitupa uwanjani kuvaana na Croatia lakini Scholes anaona ili kikosi hicho kifanye vizuri hapo mwakani basi hakina budi kuwajumuisha kikosini nyota hao ili kuongeza makali na uzoefu.

    Scholes amesema “England wanapaswa kuiga mfano wa Hispania hasa kwa kiungo Juan Mata.Mata alikuwa miongoni wa wachezaji wa Hispania walioiwezesha nchi hiyo kutwaa kombe la dunia mwaka 2010 pale Africa Kusini na akapelekwa tena kwenye kikosi cha vijana cha nchi hiyo na kukisaidia kutwaa ubingwa wa Ulaya mwaka uliofuata”


    “Kama mpango huo ulifanikiwa kwa Juan Mata kwanini usitumiwe kwa nyota tulionao?

    Alihoji Scholes na kuongeza


    “Kikosi cha vijana kikifuzu nitamshauri kocha wake Southgate awajumuishe pia Wilshere na Sterling japo wana nafasi kikosi cha wakubwa”

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SCHOLES:WILSHERE NA STERLING WARUDI KIKOSI CHA VIJANA U21 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top