728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 15, 2014

    KUZIONA SIMBA NA YANGA JUMAMOSI BUKU 7,000

    Kiingilio cha chini kwenye mechi ya
    Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya
    Yanga na Simba itakayochezwa
    Jumamosi (Oktoba 18 mwaka huu)
    Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni
    sh. 7,000.

    Washabiki watakaolipa kiingilio
    hicho ni wale watakaokaa viti vya
    rangi ya bluu na kijani ambavyo
    jumla yake ni 36,693 katika uwanja
    huo wenye viti 57,558. Viingilio
    vingine ni sh. 10,000 kwa viti vya
    rangi ya chungwa, sh. 20,000 kwa
    VIP B na C wakati VIP A itakuwa sh.
    30,000.

    Tiketi zitakazotumika kwenye mechi
    hiyo ni za elektroniki, na zimeanza
    kuuzwa jana (Oktoba 13 mwaka
    huu). Tiketi zinapatikana kwa
    mtandao wa M-PESA, CRDB
    Simbanking na maduka ya CRDB
    Fahari Huduma ambayo yapo zaidi
    ya mia moja sehemu mbalimbali
    jijini Dar es Salaam.

    Mechi hiyo namba 27
    itakayochezeshwa na mwamuzi Israel
    Mujuni Nkongo akisaidiwa na John
    Kanyenye na Ferdinand Chacha
    itaanza saa 10 kamili jioni.
    Kamishna wa mechi hiyo ni Salum
    Kikwamba kutoka mkoani
    Kilimanjaro.

    Washabiki wanatakiwa kununua
    tiketi mapema, kwani hazitauzwa
    uwanjani siku ya mechi. Milango
    yote ukiwemo ule wa upande wa
    Mbagala (Uwanja wa Ndani)
    itafunguliwa kwa ajili ya washabiki,
    na itakuwa wazi kuanzia saa 4
    asubuhi.

    Magari maalumu tu yenye stika
    ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia
    uwanjani kwa kupitia Barabara ya
    Mandela. Pia washabiki
    hawaruhusiwi kuingia uwanjani
    wakiwa na silaha, vitu vya vyuma na
    mabegi makubwa. Barabara ya
    kuingilia upande wa Chang’ombe
    itafungwa kwa watumiaji wa magari.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KUZIONA SIMBA NA YANGA JUMAMOSI BUKU 7,000 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top