728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, October 30, 2014

    PAZI AKAMILISHA DILI LA KASEJA KUTUA SIMBA

    KOCHA wa zamani wa Makipa wa Simba,
    Idd Pazi, amesema sasa ni muda mwafaka
    kwa kipa, Juma Kaseja, kurejea kwenye
    kikosi cha klabu yake hiyo ya zamani
    kutokana na uzoefu mkubwa alionao.

    Hivi karibuni kumekuwapo na taarifa za
    Kaseja kurejeshwa kwenye kikosi cha
    Simba ili akasaidiane na kipa chipukizi,
    Peter Manyika Jr pamoja na Hussein
    Shariff ‘Casillas’ kwani Ivo Mapunda
    anahusishwa na mpango wa kutemwa
    kikosini hapo.

    Pazi ambaye hivi karibuni aliondolewa
    kuinoa Simba baada ya klabu hiyo
    kushindwa kupata matokeo mazuri
    kwenye mechi za Ligi Kuu Bara, alisema
    Kaseja anaweza kuisaidia klabu hiyo
    lakini ameutaka uongozi wa kutatua
    matatizo mengine yanayochangia klabu
    hiyo kufanya vibaya.

    “Kaseja ni kipa mzoefu, ataisaidia Simba
    hivyo siyo jambo baya kumrejesha, pia
    amekuwa na historia nzuri na klabu hiyo
    kwa muda wa miaka 10 aliyokuwa pale,”
    alisema.
    “Hii pia itamsaidia Manyika ambaye
    ndiyo kwanza anakua, kuna mechi
    ambazo anaweza kudaka lakini nyingine
    ni lazima adake kipa mwenye uzoefu.”
    Akizungumzia matokeo mabaya
    yanayoikabili Simba kwa sasa, Pazi
    alisema viongozi wanafahamu kiini cha
    tatizo, lakini wamegoma kuyatafutia
    ufumbuzi jambo linaloendelea
    kuigharimu timu.

    “Kuna mambo ya nje ya uwanja ambayo
    yanachangia timu kuboronga, viongozi
    wanayafahamu lakini ni kama
    wameyafumbia macho, wajitahidi
    kuyatafutia ufumbuzi ndipo wawaze
    kufanya usajili,” alisema Pazi.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PAZI AKAMILISHA DILI LA KASEJA KUTUA SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top