728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 31, 2014

    VILABU KUKUTANA KUIJADILI QATAR

    Vilabu vikubwa barani Ulaya vitakutana wiki
    ijayo ili kutoa ombi kwa shirikisho la soka
    duniani FIFA kuandaa michuano ya dimba la
    dunia nchini Qatar kati ya tarehe 28 mwezi
    Aprili na 29 mwezi May .

    Qatar ilikabidhiwa maandalizi ya michuano
    hiyo mwaka 2010 lakini tume inayotaka
    kuliandaa dimba hilo wakati wa baridi
    imekuwa ikiendelea na kazi yake.
    Muungano wa vilabu vya Ulaya,kikiwemo
    kilabu cha Manchester,Liverpool,Barcelona na
    Bayern Munich unataka kuwasilisha ombi hilo
    ikiwemo kuanza mechi za ligi ya msimu wa
    mwaka 2021 na 2022 wiki mbili mapema na
    kucheza mechi za mwisho za kombe la FA
    baada ya fainali za dimba hilo.
    Huku Dimba la dunia likitarajiwa May
    29,hatua hiyo itasababisha kombe la FA
    nchini Uingereza kukamilika mwezi Juni.

    Muungano huo unaowakilisha timu 214 za
    bara Ulaya ,unaamini hilo huenda likaathiri
    mashindano ya mataji ya nyumbani nchini
    Ufaransa na Uhispania iwapo ombi lao
    litapuuzwa.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: VILABU KUKUTANA KUIJADILI QATAR Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top