728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, October 05, 2014

    FERDINAND:BERGKAMP ALININYIMA JEZI NIKAMCHUKIA



    Kitabu cha 2sides cha mlinzi wa klabu ya Rio Ferdinand huenda kikawa ndicho kitabu kinachoongelewa sana kwa sasa nchini England pengine kuliko vyote ambavyo vimewahi kutolewa na nyota wa mchezo wa soka.

     
    Baada ya kukosoa mbinu za aliyekuwa kocha wake katika klabu cha Manchester United David Moyes kwa kuziit za aibu kisha kudai kuwa wachezaji wa timu ya taifa ya England wanalelewa kama watoto,leo hii Ferdinand amekuja na mpya baada ya kufichua kuwa alimchukia mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Arsenal Mholanzi Denis Bergkamp kisa
    tu alikataa kubadilishana nae jezi baada ya kumalizika kwa mchezo wa ligi kuu kati yake Leeds United na Arsenal.

    Ferdinand amesema “Wakati mmoja,nikiwa bado kinda nikichezea Leeds,nilimuuliza Bergkamp Unataka kubadilishana jezi baada ya mechi?”


    Akanijibu kwa mkato “Huwa sibadilishani jezi” basi tangu hapo nikaanza kumchukia nikaacha hata tabia ya kuomba watu jezi.Nikagundua kwamba kuomba omba jezi kunawafanya watu wajione wako juu yako.
                                                                                                            
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: FERDINAND:BERGKAMP ALININYIMA JEZI NIKAMCHUKIA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top